Kamishina Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Filippo Grandi amezindua ujenzi wa nyumba zilizojengwa kwa ubunifu nchini Niger kwa lengo la kutatua mahitaji ya kibinadamu ya haraka na yanayoongezeka katika eneo la Sahel wakati suluhisho la kudumu likitafutwa kwa ajili ya wakimbizi na watu wa Niger walioko hatarini.