Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP, hii leo limekaribisha mchango wa dola milioni 3.39 kutoka mfuko wa Marekani wa maendeleo ya kimataifa USAID kusaidia kutatua hitaji la haraka la chakula kwa watu walioathirika na ukame nchini Zambia.