Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maji safi na maji taka vyote ni changamoto Nairobi Kenya

Maji safi na maji taka vyote ni changamoto Nairobi Kenya

Pakua

Uondoaji  wa maji taka na upatikanaji wa maji safi ya kunywa vyote ni changamoto kubwa ambayo inakumba sehemu  nyinyi na hasa miji ya nchi za Afrika. Kila mara mabomba ya maji taka hupasuka na kuvuja ambapo na ukarabati wa miundo mbinu muhimu kama hiyo  huchukua muda mrefu na wakati mwingine kutelekezwa kabisa. Mji wa Nairobi nchini Kenya ni miongoni mwa miji inayokubwa na changamoto hizo mbili ambazo lengo namba la maendeleo endelevu namba 6 la Umoja wa Mataifa linasisitiza  ni muhimu kwa kila mtu na kwa ajili ya maendeleo endelevu.  je kwa sasa uko katika hali gani katika suala la huduma za maji taka na maji safi ya kutumika majumbani . Mwandishi wetu wa Nairobi Jason Nyakundi amefuatilia na kuandaa makala hii.

Audio Credit
Brenda Mbaitsa/ Jason Nyakundi
Audio Duration
4'32"
Photo Credit
Picha: Kwa hisani ya James Waikibia