Fursa ya nishati mbadala yapatikana kutokana na changamoto ya magugumaji, Uganda.
Magugumaji ni changamoto inayozikabili mamlaka ya usimamizi wa rasilimali za majini yakiathiri mifumo ya maji na mazingira kwa ujumla ambayo ni msingi wa uhai na maendeleo.
Nchini Uganda kuenea kwa kasi kwa magugumaji aina ya kariba kumetishia karibu maziwa yote nchini humo kwa karibu muongo mmoja sasa.
Lakini katika utafiti wa mbinu endelevu za kukabiliana na magugu hayo, ushirikiano wa wataalam kutoka serikali ya Misri na serikali ya Uganda umewezesha utekelezaji wa mradi wa majaribio kwenye maziwa ya Kyonga na Albert ambapo magugu haya yanatumika kama nyenzo za kuzalisha gesi ya kupikia kwa mfumo teknolojia ya biogesi.
Pata maelezo zaidi katika makala iliyoandaliwa na mwandishi wetu John Kibego kutoka Uganda baada ya kutembelea wanufaika wa mradi huo kwenye ziwa Albert.