Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kukomesha usafirishaji haramu ni jukumu la dunia nzima:UN

Kukomesha usafirishaji haramu ni jukumu la dunia nzima:UN

Pakua

Usafirishaji haramu wa binadamu ni uhalifu mbaya kabisa na unagusa kila pembe ya dunia, huku waathirika wakubwa wakiwa ni wanawake, wasichana na watoto umesema leo Umoja wa Mataifa. Arnold Kayanda na ripoti kamili. 

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya uhalifu na madawa UNODC ,katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupinga usafirishaji haramu wa binadamu, asilimia 72 ya waathirika wa uhalifu huu ni wanawake na wasichana huku idadi ya watoto waliothirika ikiongezeka mara mbili tangu mwaka 2004 hadi 2016.

Audio Credit
UN News/Arnold Kayanda
Audio Duration
3'55"
Photo Credit
© UNICEF/UNI91025/Noorani