Mjasiriamali ageuza taka kuwa vifaa vya ujenzi nchini kenya
Lengo nambari 13 la malengo ya maendeleo endelevu SDG’s au ajenda ya 2030, linahimiza Umoja wa Mataifa ya mashirika yake kuweka msisitizo katika utekelezaji wa ulinzi wa mazingira ikiwa ni pamoja na utokomezaji wa matumizi ya bidhaa za plastiki.
Serikali nchini Kenya imekuwa mstari wa mbele katika kuzishirikisha asasi za kiraia katika mapambano haya dhidi ya matumizi ya plastiki, ambapo wadau mbalimbali wameitikia wito huo kwa kuanzisha miradi yenye lengo la kujiajiri lakini pia kulinda mazingira.
Mwandhisi wetu Jason Nyakundi kutoka Kenya amefanya amekutana na DKT. Aghan Oscar, mshindi wa tuzo mbalimbali zilizotokana na mradi wake aliounzinsha miaka 20 iliyopita wa kubadili taka za kila aina na kutengeneza vifaa vya ujenzi, mkaa na mbolea . Kwa undani zaidi kuhusu jitihada zake unagane nao katika makala hii.