Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Harakati za wanawake kusaka sauti katika Kaunti ya Kisii nchini Kenya.

Harakati za wanawake kusaka sauti katika Kaunti ya Kisii nchini Kenya.

Pakua

Umoja wa Mataifa na mashirika yake kwa pamoja wamekuwa mstari wa mbele kupigia  chepuo suala la usawa kijinsia katika kila jamii hususan katika nafasi ya  uongozi ili kuhakikisha mwanamke anapewa nafasi katika maendeleo ya jamii yake.

Nchini Kenya kama ilivyo pia katika mataifa mengine duniani, juhudi za kumwinua mwanamke zinaendelea japokuwa katika baadhi ya maeneo bado nafasi  ya  mwanamke inazidi kukandamizwa katika nyanja ya maamuzi hivyo kupelekea ajenda ya kumkomboa mwanamke kutopewa kipaumbele katika miswada mbalimbali bungeni.

Flora Nducha wa Idhaa ya kiswahili alipata fursa na kuzungumza na Bi Karen Magala ambaye ni mwenyekiti wa wanawake katika bunge la kaunti ya Kisii nchini Kenya . Katika mahojiano yao kandoni mwa mkutano wa hali ya wanawake CSW63 jijini New York, Bi Magala  anaanza kwa kueleza changamoto wanazokabiliana nazo.

Audio Credit
Arnold Kayanda/Flora Nducha
Audio Duration
4'4"
Photo Credit
Photo IRIN/Aubrey Graham