“Kenya tumepiga hatua katika nishati mbalala kuliko wakati wowote ule tangu uhuru” - Elmi
Umoja wa Mataifa kwa ushirikiano na asasi mbalimbali za kiaraia, pamoja na serikali wamekuwa mstari wa mbele kutekeleza ahadi ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030.
Lengo nambari 7 ni moja kati ya malengo ya maendeleo endelevu SDGs, yanayotoa fursa kwa serikali , na mahirika ya Umoja wa Maitaifa kuwawezesha wananchi kupata nishati mbadala kwa bei nafuu lengo likiwa kuwakomboa lakini pia kulinda mazingira.
Nchini Kenya serikali kupitia wizara ya misitu na mazingira imepiga hatua kubwa katika kutimiza hilo tangu ilipoanzisha uzalishaji wa nishati mbadala miaka mitano iliyopita.
Akifafanua utekelezaji huo katika Makala hii si mwingine bali Muhamed Elmi katibu tawala wa wizara ya misitu namazingira Kenya wakati wa mahojiano na kutuo cha habari cha Umoja wa Mataifa jijini Nairobi UNIC.