Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tanzania na mbinu bunifu za kuboresha huduma za afya kwa wanawake na watoto.

Tanzania na mbinu bunifu za kuboresha huduma za afya kwa wanawake na watoto.

Pakua

Ni mkutano ambao umewaleta pamoja takribani washiriki 9000 kutoka nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa. Kuanzia nchi za kipato cha juu, kati na cha chini ili kila mmoja apate kujifunza kutoka kwa mwingine. Na katika tukio lililoandaliwa na Tanzania kandoni mwa mkutano huo ndipo Dkt Ellen Mkondya Senkoro, Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi ya Benjamin Mkapa na Wakili Haika Harrison Ngowi wa shirika la Save the Children katika mahojiano haya na Arnold Kayanda  wameieleza UN News Kiswahili kile ambacho wamekuja kubadilishana na wenzao wa mataifa mengine. 

Audio Credit
Assumpta Massoi/Arnold Kayanda
Audio Duration
5'40"
Photo Credit
CCBRT/Dieter telemans