Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Restless Development yazidi kuchagiza jamii kuhusu madhara ya ukatili wa jinsia

Restless Development yazidi kuchagiza jamii kuhusu madhara ya ukatili wa jinsia

Pakua

Ukatili wa jinsia ni suala ambalo limekuwa kikwazo kwa  maendeleo ya jamii hasa kwenye maeneo ambako mfumo dume umeshamiri na wanawake wanakumbwa na ukatili huo katika njia mbalimbali. Umoja wa Mataifa unatambua kuwa ukatili wa jinsia ni kikwazo na ndio maana unapigia chepuo usawa wa jinsi na kutokomeza mila potofu na hata sheria ambazo kwa njia moja au nyingine zinashamirisha ukatili wa jinsia. Hata hivyo changamoto ni pale ambapo jamii inakuwa ina uoga au hata pengine hawatambua kuwa kitendo fulani ni ukatili wa jinsia. Ni kwa kuzingatia hilo shirika la kiraia la Restless Development lina vijana waleta mabadiliko ambao wanapita mashinani kuelimisha umma kuhusu ukatili wa jinsia na miongoni mwao ni Thobias Komba ambaye anatoka Dodoma mkoani Tanzania na hivi sasa yuko jijini New  York, Marekani akihudhuria  mkutano wa 63 wa kamisheni ya hali  ya wanawake duniani, CSW. Assumpta Massoi amezungumza naye na kumuuliza pamoja na mambo mengine hatua ambazo wanachukua kuelimisha umma kuhusu ukatili wa jinsia zinazaa matunda na je jamii inaitikia?

Audio Credit
Arnold Kayanda/Assumpta Massoi
Audio Duration
3'46"
Photo Credit
UN/Assumpta Massoi