Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanawake Afrika Mashariki waleta maendeleo katik jamii husika

Wanawake Afrika Mashariki waleta maendeleo katik jamii husika

Pakua

Dunia ikiadhimisha siku ya wanawake duniani masuala mengi yameangaziwa, ikiwemo umuhimu wa kumwezesha mwanamke lakini suala ambalo ni la msingi na wakati mwingine halimulikwi ni mchango wa wanawake wenyewe katika kujikwamua na hata kuikwamua jamii kupitia shughuli wanazozifanya.

Ni kwa kuzingatia hilo ambapo leo tunamulika wanawake watatu kutoka nchi za Afrika Mashariki. Licha ya kuwa wametoka nchi tofauti lakini wanawake hawa wamejizatiti kuboresha sio tu maisha yao bali pia kuinua jamii zao kwa ujumla kwa kutumia mbinu mbalimbali. 

Audio Credit
Grace Kaneiya
Audio Duration
5'9"
Photo Credit
UN Women/Carlos Rivera