Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Msaada zaidi kwa Tanzania wahitajika ili ihudumie vyema wakimbizi- Grandi

Msaada zaidi kwa Tanzania wahitajika ili ihudumie vyema wakimbizi- Grandi

Pakua

Kamishna Mkuu wa shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa ,UNHCR, Filippo Grandi amehitimisha ziara yake ya siku nne nchini Tanzania akitoa wito kwa jamii ya kimataifa kuwekeza zaidi mikoa ya kaskazini-magharibi mwa nchi hiyo ambayo ni nyumbani kwa wakimbizi 330,000. 

Ziara hiyo ya siku nne ilimfikisha Bwana Grandi kwenye kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma nchini Tanzania ambako alishuhudia jinsi wakimbizi walivyo na matumaini licha ya kuishi ugenini.

Akiwa kambini alikutana na mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Selemani Boaz ambaye ni mchuuzi kambini humo na akimweleza kuwa soko hilo linasaidia utangamano na wenyeji na pia wakimbizi wanapata vyakula tofauti na vile vya msaada.

Audio Credit
Grace Kaneiya
Audio Duration
1'59"
Photo Credit
UNHCR/Georgina Goodwin