23 Januari 2019
Pakua
Hii leo tunaanzia huko Sudan ambako sintofahamu ya mustakabali wa watoto kwenye ghasia zinazoendelea imesababisha UNICEF kupaza sauti yake. Huko Jordan ILO yasaidia wakimbizi kutoka Syria na wenyeji raia wa Jordan kupata ajira zenye hadhi na utu. Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, manusura wa ebola sasa nao wasimama kidete kunusuru wagonjwa, kulikoni? makala tunakwenda Burundi, vijana washtuka sasa wajikwamua kiuchumi badala ya kusubiri serikali. Mashinani ni masuala ya hifadhi ya jamii na changamoto wanazokumbana nazo vibarua! Karibu na mwenyeji wako ni Arnold Kayanda
Audio Credit
Arnold Kayanda
Audio Duration
11'52"