Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanafunzi Hoima wapaza sauti dhidi ya ukatili wa kijinsia

Wanafunzi Hoima wapaza sauti dhidi ya ukatili wa kijinsia

Pakua

Hatimaye siku 16 za kupiga vita na kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa mwaka huu wa 2018 zimefikia tamati ambapo maeneo mbalimbali duniani yametamatisha kampeni hiyo kwa matukio tofauti. Mathalani huko nchini Uganda kwenye makazi ya wakimbizi wa Kyangwali mjini Hoima Magharibi mwa Uganda, wanafunzi walishiriki kwenye kilele cha maadhimisho hayowakielezea aina ya visa vya ukatili, wanaotekeleza na kile ambacho kinapaswa kufanyika, kama anavyosimulia mwandishi wetu nchini humo John Kibego aliyehudhuria shamrashamra hizo.

Audio Credit
Siraj Kalyango/John Kibego.
Audio Duration
3'38"
Photo Credit
UN Photo/Herve Serefio