Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utamaduni wa jamii yako ni haki  yako, lasema tamko la haki za binadamu la UN

Utamaduni wa jamii yako ni haki  yako, lasema tamko la haki za binadamu la UN

Pakua

Katika mwendelezo wa uchambuzi wa ibara kwa ibara za tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa leo tunamulika ibara ya 27 inayosema kuwa kila mtu ana haki ya kushiriki na kunufaika na tamaduni, sanaa na sayansi ya jamii yake. Hii imenyumbuliwa katika pande mbili ambapo ili kuweza kupata ufafanuzi wa kisheria Grace Kaneiya wa Idhaa hii amezungumza na Dkt. Elifuraha Laltaika, mhadhiri wa sheria kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira nchini Tanzania na anaanza kwa kufafanua yaliyomo.

 

Audio Credit
Arnold Kayanda/Grace Kaneiya
Audio Duration
2'2"
Photo Credit
UN/Eskinder Debebe