Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkimbizi bila elimu ni sawa na mti bila matunda:Mkimbizi Rachel

Mkimbizi bila elimu ni sawa na mti bila matunda:Mkimbizi Rachel

Pakua

Elimu kwa mkimbizi ni muhimu sana, kwani bila elimu huwezi fanya chochote , iwe ni kwa upande wa ajira au hata ujasiriliamali, unakuwa sawa na mti usiozaa matunda ambao huonekana kutokuwa na faida yoyote. Kauli hiyo ni ya mmoja wa wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidekrasia ya Congo DRC, ambaye aliishi na kusomea kambini nchini Uganda. Akizungumza na mwandishi wetu John Kibego kuhusu haki ya kila mtu kupata elimu bila kujali kabila, rangi au uraia wake kama ilivyoainishwa kwenye Ibara ya 26 ya tamko la haki za binadamu, anasema haijalishi mazingira uliyopo “elimu ni elimu”.

Audio Credit
Siraj Kalyango/ John Kibego
Audio Duration
3'32"
Photo Credit
UNICEF/UN0153963/Obadi