Jamaica yafurahi muziki wake wa mtindo wa Reggae kutambuliwa na UNESCO
Pakua
Muziki mbali na kuelimisha, kufahamisha, kuliwaza ama kuburudisha lakini pia kwa upande mwingine ni tunu inayotumika kutambulisha jamii ya eneo fulani kwa wakati fulani. Kupitia muziki, jamii kutoka upande mmoja inaweza kufahamu utambulisho wa mwingine na imefika wakati hata jamii moja kuiga tamaduni hiyo, mathalani muziki wa mtindo wa reggae kutoka Jamaica, ambao sasa umeenea kote duniani hadi umetambuliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni-UNESCO kama turathi za tamaduni zisizogusika za kibinadamu. Je ni kwa vipi? wenyewe wajamaica wanasemaje? Kwa undani zaidi kuhusu hilo ungana na Siraj Kalyango katika makala ifuatayo.
Audio Credit
Priscilla Lacomte/ Siraj Kalyango
Audio Duration
1'27"