Mara nyingi haki za watu wengi hubinywa kutokana na sababu kama vile, vita, mfumo wa utawala na hata mgawanyiko katika jamii.
Pakua
Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa Ibara ya 6 inasema “kila mtu anayo haki, binafsi au kwa ushirikiano na wengine, kuanzisha na kujadili dhana na kanuni mpya za haki za binadamu na kuzitetea ili zikubalike.” Lakini mara nyingi watu hawapati fursa ya kufanya hivyo na hata wakiiipata haki hizo hubinywa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo, vita, mfumo wa utawala na hata mgawanyiko katika jamii. Mtaalam huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu nchini Somalia Bwana Tom Bahame Nyanduga amemueleza Flora Nducha wa Idhaa hii changamoto zinazochangia ukiukwaji huo kwa nchi kama Somalia iliyoghubikwa na vita kwa zaidi ya miongo mitatu sasa. Anaanza kwa kufafanua haki zenyewe
Audio Credit
Flora Nducha
Audio Duration
4'31"