Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kilimo bora chaimarisha kipato cha kaya Vietnam

Kilimo bora chaimarisha kipato cha kaya Vietnam

Pakua

Kilimo ni shughuli inayoleta maendeleo siyo tu kwa kijiji, eneo au taifa kwa ujumla bali pia kwa mtu binafsi na familia yake. Ni kwa kuzingatia hilo, Umoja wa Mataifa umekuwa kila mara unakipigia upatu na kukijumuisha katika ufanikishaji wa  baadhi ya  malengo ya maendeleo endelevu, kama vile malengo namba moja la kuondoa umaskini na pia namba 2 la kutokomeza njaa bila kusahau lengo namba nane  la  kazi nzuri na ukuaji wa kiuchumi na vilevile   usawa wa kijinsia ambalo ni lengo namba tano.

Kwa mantiki hiyo kilimo ambacho ni endelevu kimechukuliwa kwa makini nchini Vietnam ambako kimesaidia mkulima mmoja mwanamke kupata mavuno bora ya chai. Kilimo endelevu ambacho hakiharibu mazingira kimemfanya mkulima huyo NGUYEN  THI THANH  kuona nuru kwenye maisha  yake. Je nini kimefanyika. ungana basi na Siraj Kalyango katika makala ifuatayo.

Audio Credit
Anold Kayanda/Siraj Kalyango
Sauti
2'52"
Photo Credit
Wanawke wakichuma majani katika eneo la Mbeya, Tanzania(Picha ya UM/B Wolff)