Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Naona mustakabali mkubwa ambao unaongozwa na vijana-Restless Development

Naona mustakabali mkubwa ambao unaongozwa na vijana-Restless Development

Pakua

Umoja wa Mataifa Jumatatu hii umezindua mkakati wake mpya kuhusu vijana ukilenga kuimarisha mchango wa takribani vijana bilioni 2 duniani  kwa lengo la  kukuza amani, uadilifu pamoja na kuwa na  dunia endelevu. Mkakati huo umepatiwa jina,  “Vijana 2030:Mkakati wa  Umoja wa Mataifa  kwa vijana,”  umeshuhudiwa  na viongozi wa nchi na wakuu wa serikali, lakini pia vijana ambapo mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo la kihistoria kutoka shirika la kiraia la Restless Development amezungumza na Grace Kaneiya wa Idhaa hii punde tu baada ya tukio hilo na anaanza kwa kujitambulisha.

Soundcloud
Audio Credit
Siraj Kalyango/Grace Kaneiya
Audio Duration
3'48"
Photo Credit
UN Photo/Mark Garten)