Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanawake Burundi wapata mwamko kujiendeleza kiuchumi

Wanawake Burundi wapata mwamko kujiendeleza kiuchumi

Pakua

Huko Burundi, wanawake wameanza kuchangamkia biashara ndogondogo ili kustaawisha  familia zao.Takwimu zinaonyesha kuwa asimilia 53 ya raia wa nchi hiyo ya Burundi ni wanawake, lakini bado  changamto kubwa ni umaskini unaowazingira sehemu  kubwa ya wanawake hao pamoja  na shida za  kiuchumi. 

Lakini kuna nuru gizani kwani wanawake  hao sasa wameanza kugundua kwamba kusubiri kushikwa mkono sio  rahisi. Na ni bora kufikiria wenyewe kwanza  chanzo  cha kujiendeleza  na kustaawisha familia zao. Mwandishi wetu wa Maziwa Makuu Ramadhani Kibuga amezungumza na wanawake hao katika soko mojawapo mjini Bujumbura na kupokea hisia zao ambapo Siraj Kalyango anasimulia katika makala ifuatayo.

 

 

Audio Credit
Grace Kaneiya/Siraj Kalyango
Audio Duration
4'14"
Photo Credit
FAO/Cristina Aldehuela