Demistura asema katiba ndiyo itaweka mambo sawa Syria
Pakua
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Syria, Staffan de Mistura, amesema anatarajia kukutana na maafisa wa ngazi ya juu wa Urusi, Uturuki na Iran mnamo Septemba 10 na 11 , katika majadiliano ya muendelezo wa mikutano iliyofanyika Geneva na Sochi hapo awali.
Akizungumza na waandishi wa habari hii leo mjini Geneva Uswisi, de Mistura amesema kuunda kamati ya kusimamia mabadiliko ya katiba Syria ndio mtihani.
Audio Credit
Grace Kaneiya
Audio Duration
2'5"