Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

14 Agosti 2018

14 Agosti 2018

Pakua

Katika jarida hii leo Assumpta Massoi anaangazia yafuatayo:

  1. Jamii ya kabila dogo huko nchini Libya, yafurushwa kutoka makazi yao ya muda, wanawake na wasichana watishiwa kubakwa, hivi sasa wengine wanaishi kwenye magari, UNHCR yapaza sauti.
  2. Sasa wakimbizi hawapaswi kuhofia tena iwapo hawafahamu lugha ya kigeni  kule wanakohamia kwa kuwa wasomi wawili kutoka Chuo Kikuu kimoja nchini Marekani wamekuja na apu itendayo miujiza, wewe nawe waweza kujitolea kusaidia kwa kuwa mkalimani au mtafsiri.
  3. Jamii za asili ni lazima ziangaliwe kwa jicho la kipekee katika kupima na kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, amesema Dkt. Elifuraha Laltaika kutoka Tanzania
  4. Na makala Patrick Newman amebisha hodi  nchini Lesotho, wanawake huko hawataki mchezo katika kukabiliana na umaskini.
  5. Mashinani ni Tanzania, mradi wa UNICEF waleta kicheko kwa wazazi wa wanafunzi mkoani Mbeya, Karibu!
Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
9'58"