Ushairi una dhima kubwa katika ustawi wa binadamu
Pakua
Ushairi licha ya kuwa moja ya fasihi zinazoburudisha, huendana pia na baadhi ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ya Umoja wa Mataifa. Miongoni mwa malengo hayo ni lile la 16 linalogusia amani, haki, ujumuishi na utangamano baina ya jamii za makabila na imani tofauti. Mtunzi huzingatia kile kinachomsukuma ilhali mgani naye hughani shairi kwa mbwembwe ili kufikisha ujumbe husika.Ni katika muktadha huo katika moja ya kusanyiko la kidini huko London, nchini Uingereza hivi karibuni, ushairi ulitumika kufikisha ujumbe na Siraj Kalyango alihudhuria na kuandaa Makala hii.
Audio Credit
Flora Nducha/Siraj Kalyango
Audio Duration
3'44"