Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ndoto zilizoingia katika mashaka ukimbzini, Uganda.

Ndoto zilizoingia katika mashaka ukimbzini, Uganda.

Pakua

Vijana  ndio nguzo za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, kwani ndio viongozi wa sasa na  wa hapo baadaye. Lakini wengi wanakabiliwa na  changamoto za kuweza kufanya vitu ambavyo vitawafaa hapo baadaye. Hali ya vijana katika mataifa yanayaoinukia ni ya shida mno. Hii ni kwa kuwa hujikuta ndoto zao za kujiendeleza wakati mwingine zinakwama kabisa na huenda si kwa sababu za kujitakia.

Kijana  mmoja kwa jina la Tango Patrick,ni  mkimbizi kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congoambaye sasa anaishi Uganda na anapenda sana kuimba na mara kwa mara  wanaburudisha wakimbizi wenzake , kimuziki ,wakati wa sherehe mbalimbali licha ya changamoto  kadhaa kama za kifedha  ambazo zinakwamisha ndoto yake ya kuwa mwanamuziki nyota sio tu katika kanda ya Afrika Mashariki na kati lakini  pia na duniani kote.

Ili kujua undani wa ndoto ya kijana huyo tuungane na mwandishi wetu wa Uganda John Kibegoambaye alikutana naye katika makaazi   ya wakimbizi ya Nakivale magharibi mwa Uganda. Anaanza kwa kumpa kionjo .

Audio Credit
Siraj Kalyango/John Kibego
Sauti
3'45"
Photo Credit
Picha: UM/Video capture