Taasisi za kidini Tanzania zina mchango mkubwa wa kufanikisha SDG’s:Dr Mbando
Pakua
Taasisi za kidini nchini Tanzania zina mchango mkubwa wa kusaidia kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu yaani SDG’s kwa kutoa huduma mbalimbali zikiwemo za kiafya.
Hayo yameelezwa na dr. Zebadia Mbando mkurugenzi wa tiba katika taasisi ya dini ya kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) mjini Arusha. Kwa miaka mingi taasisi hiyo yenye hospitali , vituo vya afya na zahanati zaidi ya 200 nchini Tanzania imekuwa ikitoa huduma za afya kwa maelfu ya watu hususani wa vijijini. Na leo katika sehemu ya pili ya mahojiano , Flora amemuuliza Dr. Mbando huduma za afya zinazotolewa na taasisi yao ikiwemo huduma ya shufaa zinamgharimu mwananchi kiasi gani?
Audio Credit
Grace Kaneiya/ Flora Nducha
Sauti
3'25"