Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanawake Burundi tumetoka mbali,japo bado kuna changamoto:Nzeyimana

Wanawake Burundi tumetoka mbali,japo bado kuna changamoto:Nzeyimana

Pakua

Wanawake nchini Burundi wamepiga hatua kubwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo masuala ya uongozi baada ya serikali kuwahakikishia uwakilishi wa asilimia 30 bungeni.

Hata hivyo bado kuna changamoto katika kutimiza malengo ya maendeleo  endelevu SDG’s yahusuyo wanawake kama usawa wa kijinsia, elimu, haki za kurithi na fursa za kiuchumi hususan wale waishio vijijini.

Katika makala hii mwandishi wetu wa maziwa Makuu Ramadhani KIBUGA ameketi na kuzungumza na mbunge wa Burundi katika  bunge la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki Leontine Nzeyimana  kutathimini hali ya mwanamke nchini humo .

Audio Credit
Siraj Kalyango/Ramadhani Kibuga
Audio Duration
4'27"
Photo Credit
PICHA: UNHCR/Maktaba/Eduardo Soteras Jalil