Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tanzania na mpango shiriki wa uhifadhi wa misitu

Tanzania na mpango shiriki wa uhifadhi wa misitu

Pakua

Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya misitu duniani imezitaka serikali kuchukua hatua jumuishi katika ulinzi na uhifadhi wa misitu ili kupunguza kasi ya kupungua kwa eneo la misitu kila uchao. 

Kwa mujibu wa shirika la chakula na kilimo duniani, FAO ambalo ndio mwandishi wa ripoti hiyo, hatua kama vile kupunguza ukataji miti holela, matumizi endelevu ya misitu na kupanda miti ni hatua ambazo zinapaswa kutekelezwa kwa kutumia jamii zinazonufaika na rasilimali za misitu.

Mkurugenzi Mkuu wa FAO José Graziano da Silva amesema hatua hizo ni muhimu kwa kuzingatia kuwa misitu ni rasilimali adhimu kwa vipato na uhai wa binadamu, akisema misitu bora ni muhimu kwa kilimo endelevu na maji bora.

Kwa mantiki hiyo ripoti inasisitiza umuhimu wa kuwepo kwa mifumo ya uwazi ya haki za kumiliki misitu na kushirikisha jamii.

Nchini Tanzania tayari hatua zimeanza kuchukuliwa kulinda misitu ikiwemo kushirikisha jamii kama anavyoeleza Dkt. Ezekiel Mwakalukwa, Mkurugenzi wa Idara ya misitu na Nyuki kwenye wizara ya maliasili na utalii ya nchi hiyo.

Ripoti hii mpya imeandaliwa kuelekea jukwaa la ngazi ya juu la Umoja wa Mataifa kuhusu maendeleo endelevu litakalofanyika jijini New York, Marekani tarehe 9 mwezi huu.

Audio Credit
John Kibego
Audio Duration
1'47"
Photo Credit
UNMISS/Eric Kanalstein