Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Madhara ya mifuko ya plastiki ni gharama kubwa kwa wakaazi Bujumbura

Madhara ya mifuko ya plastiki ni gharama kubwa kwa wakaazi Bujumbura

Pakua

Mifuko ya plastiki imekuwa kero kwani ina madhara makubwa siyo tu kiafya bali pia kimazingira. Imesababisha kuziba kwa mifereji ya majitaka na huko kwenye maji  ikiathiri pia viumbe vya majini. Barani Afrika kuna nchi ambazo zimepitisha sheria kutokomeza matumizi ya mifuko ya plastiki kwa mfano Kenya na Rwanda na nyingine zikiweka mikakati kufikia hilo.

Serikali ya Burundi nayo imeanzisha mchakato unaonuwia baadaye  kupiga marufuku  matumizi ya mifuko ya plastiki. Kwa hatua ya kwanza maafisa wa serikali na watetezi wa  mazingira wameanza  kutoa mafunzo kuhusu madhara ya  kimazingira ya kutumia mifuko hiyo ya plastiki.Lakini changamoto kubwa ni kukosekana kwa mbadala ili kuweza kuachana na mifuko hiyo. Je nini kinafanyika zaidi na wananchi wanasemaji? Basi tuungane na mwandishi wetu wa Maziwa Makuu Ramadhani Kibuga ametuandalia makala haya akiwa mjini Bujumbura.

Audio Credit
Grace Kaneiya/ Ramadhani Kibuga
Audio Duration
4'26"
Photo Credit
Picha: Kwa hisani ya James Waikibia