Japo wapo ugenini, bado fedha zao ni muarobaini
Pakua
Kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD, imesema fedha zinazotumwa na wahamiaji walioko ughaibuni zimekuwa mkombozi kwa mataifa mengi ya Afrika.
Mathalani kati ya mwaka 2014 na 2016 wahamiaji walioko ughaibuni walituma jumla ya dola bilioni 65 kwa nchi za Afrika.
Afisa katika ofisi ya UNCTAD, huko Geneva, Uswisi, Jane muthumbi akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa ametaja baadhi ya nchi nufaika zaidi ikiwemo Liberia ambayo asilimia 27 ya pato la nchi hutokana na fedha zinazotumwa na wahamiaji.
Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
1'18"