Katu sitaki kurejea DRC, naogopa vita- Kijana mkimbizi
Pakua
Mchango wa vijana katika masuala mbalimbali ni dhahiri ili kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu. Hata hivyo mapigano na vita katika baadhi ya nchi ikiwemo Afrika imesababisha vijana kukimbia nchi zao na kusaka hifadhi nchi jirani. Wengine sasa hata hawataki kurejea nyumbani na mchango wao uko mashakani.
Katika kuangazia mchango wa vijana katika jamii tunaelekea kambi ya Kyangwali huko Hoima nchini Uganda ambapo John Kibego amezungumza na vijana wakimbizi kuhusu utumikishaji na ukatili dhidi ya watoto na vijana.
Audio Credit
John Kibego
Audio Duration
3'10"