Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana tutumie fursa zilizopo kujikwamua na umasikini: Majd

Vijana tutumie fursa zilizopo kujikwamua na umasikini: Majd

Pakua

Tatizo la ajira katika nchi zinazokabiliwa na  machafuko ya kivita ni kikwazo kikubwa  kwa maendeleo ya  vijana, kwa sababu wahalifu, waasi na watu wenye  itikadi kali hutumia  mwanya huo na  kuwarubuni vijana hao  kujiingiza katika ugaidi na uwaasi. 

Umoja wa Mataifa kupitia mashirika yake kama ILO na wadau, wamekuwa bega kwa bega na serikali nyingi duniani  kutafuta mbinu za kuwawezesha vijana kujikwamua na  tatizo la ukosefu wa ajira kupitia ufadhili wa miradi ya vijana, mafunzo ya ujasiriamali ili kuwawezesha vijana kufikia  lengo nambari 8 la ajenda ya maendeleo endelevu  linalozungumzia ajira bora na ukuaji wa uchumi.

Kwa muktadha huo, mwandishi wetu leo anatupeleka katika mji wa Gaza, huko Palestina ambako msichana mmoja amekuwa chachu na mfano wa kuigwa na jamii yake baada ya kutumia  ubunifu wake na kuanzisha miradi ambayo imewapa wananchi wa Gaza matumaini mapya katika masuala ya ujenzi na nishati mbadala. Nini kilichojiri huko?

Ungana na Patrick Newman katika makala hii, upate undani zaidi.

Audio Duration
4'49"
Photo Credit
Wanawake na watoto wa maeneo yaliyokaliwa ya Palestina.(Picha:UM/Maktaba/Shareef Sarhan)