Ukimtunza ngombe wako, maziwa hayakupigi chenga
Umoja wa Mataifa na mashirika wenza wamekuwa mstari wa mbele katika kuwawezesha wanawake vijijini katika programu za ujasiriamali kwa ushirikiano na serikali mbalimbali duniani kote.
Nchini Bangladesh Serikali kwa ushirikiano na shirika la chakula na kilimo FAO wameendelea kuwasaidia wanawake wa vijijini kupitia miradi ya kilimo na ufugaji ili kuwawezesha kijikwamua na umaskini kama ilivyo katika agenda ya maendeleo enedelevu ya mwaka 2030.
kwa muktadha huo, mwandishi wetu Patrick Newman anatupeleka katika kijiji cha Panjor Bhanga kaskazini mwa Bangladesh ambako mwanamke mmoja mjasiriamali na mfugaji aliyenufaika na mafunzo ya ujasiriamali amekuwa kivutio cha wengi kutokana na mafanikio aliyoyapata katika shughuli zake za kimaendeleo. nini kilichojiri? Unagana naye katika makala hii.