Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

OPCW yathibitisha matumizi ya sumu ya kemikali Salisbury

OPCW yathibitisha matumizi ya sumu ya kemikali Salisbury

Pakua

Shirika la kudhibiti silaha za kemikali, OPCW limethibitisha matumizi ya kemikali ambayo Uingereza ilitaja kuwa imetumika kwenye tukio la tarehe 4 machi mwaka huu huko Salisbury, Uingereza. 

OPCW iliombwa na Uingereza kufanya uchunguzi huo ambao katika tukio hilo aliyekuwa jasusi wa Uingereza na Urusi Sergei Skripal na binti yake waliwekewa kemikali hiyo ya sumu.

Dkt. Ahmet Ahmet Üzümcü ambaye ni Mkurungezi Mkuu wa OPCW ameshukuru maabara ya chombo hicho iliyoteuliwa kuchunguza sampuli ya kemikali iliyotumiwa ili kubaini ukweli kuhusu matumizi ya kemikali hiyo.

Ujumbe wa Uingereza kwenye OPCW uliomba kuwa sekretarieti ya chombo hicho iwasilishe ripoti ya matokeo ya uchunguzi kwa nchi zote wanachama zilizotia saini mkataba wa kutokomeza silaha za kemikali, CWC na kuandaa ripoti fupi itakayochapishwa hadharani.

Sakata hilo la matumizi ya kemikali ya sumu dhidi ya jasusi hiyo na binti yake lilijadiliwa wiki iliyopita kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambapo wawakilishi wa Urusi na Uingereza walishutumiana juu ya suala hilo.

Audio Credit
Flora Nducha
Audio Duration
1'7"
Photo Credit
Mavazi ya kujikinga dhidi ya kemikali za sumu.(Picha:OPCW)