Haiti inaendelea kuimarika hatua kwa hatua-Lacroix
Operesheni ya usaidizi wa ujenzi mpya nchini Haiti itafanikiwa tu endapo uhusiano kati ya serikaliya nchi hiyo na na operesheni mpya ya ujenzi ukiwa mzuri.
Hayo yamesemwa na mkuu wa operesheni za ulinzi wa Amani za umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix, wakati akihutubia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hatua zinazoendelea Haiti.
Lacroix amelielezea baraza hilo kuhusu ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,kuhusu operesheni mpya ya ambayo itaisaidia pia Haiti kisheria ijulikanayo kamaMINUJUSTH.
Bwana Lacroix amesisitiza kuwa uhusiano mzuri kati ya pande hizi mbili unafaa uegemee mshikamano na kuaminiana ili kuweza kufanikiwa katika malengo ya kuliinua tena taifa hilo lililopitia misukosuko mingi ikiwemo tetemeko la ardhi, mlipuko wa kipindupindu n ahata hatihati ya kisiasa..
Hii ndiyo mara ya kwanza , kwa mujibu wa Larcoix, baraza linajadilia operesheni mpya ya Umoja wa Mataifa ya kusaidia Haiti kwa masuala ya kisheria, MINUJUSTH, tangu ianzishwe Oktoba mwaka jana 2017.
Pia ametaja baadhi ya mambo ambayo yamefanyika kufikia sasa katika juhudi za kuisadia Haiti kufufua mfumo wa sheria ikiwa ni pamoja na kubadili baadhi ya vipengele vya katiba. Ameongeza kuwa opereshi ya sasa ya Umoja wa Mataifa inafanya kazi zake kama kawaida japo kuna matatizo ya hapa na pale.
Amesema kuwa maafisa wa kikosi hicho, raia wa kawaida, wamejikita katika mji mkuu wa Port- au -Prince huku timu zingine ndogondogo za kuhamahama zikichunguza hali ya kisiasa na utawala wa sheria zinazurura mikoa yote 10 huku maafisa wake wakiwasiliana na wananchi pamoja na washika dau wengine.
Pia kikosi cha Umoja wa Mataifa kimetuma maafisa wake sio tu katika vikosi vya polisi lakini pia katika magereza 18 nchini humo.
Amesema kuwa eneo ambalo wametilia mkazo ni kusaidia kukabiliana na watu kuwekwa ndani bila kufikishwa mahamani na vilevile mjazo gerezani.
Hata hivyo ameongeza kuwa tatizo baado ni udhaifu katika taasisi za sheria kuendelea kuzusha changamoto kwani kuna baadhi watu ambao hawaguswi kwa kuchukua hatua za kinidhamu dhidi endapo wametenda makosa.
Hayo yamesemwa na mkuu wa operesheni za ulinzi wa Amani za umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix, wakati akihutubia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hatua zinazoendelea Haiti.
Lacroix amelielezea baraza hilo kuhusu ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,kuhusu operesheni mpya ya ambayo itaisaidia pia Haiti kisheria ijulikanayo kamaMINUJUSTH.
Bwana Lacroix amesisitiza kuwa uhusiano mzuri kati ya pande hizi mbili unafaa uegemee mshikamano na kuaminiana ili kuweza kufanikiwa katika malengo ya kuliinua tena taifa hilo lililopitia misukosuko mingi ikiwemo tetemeko la ardhi, mlipuko wa kipindupindu n ahata hatihati ya kisiasa..
Hii ndiyo mara ya kwanza , kwa mujibu wa Larcoix, baraza linajadilia operesheni mpya ya Umoja wa Mataifa ya kusaidia Haiti kwa masuala ya kisheria, MINUJUSTH, tangu ianzishwe Oktoba mwaka jana 2017.
Pia ametaja baadhi ya mambo ambayo yamefanyika kufikia sasa katika juhudi za kuisadia Haiti kufufua mfumo wa sheria ikiwa ni pamoja na kubadili baadhi ya vipengele vya katiba. Ameongeza kuwa opereshi ya sasa ya Umoja wa Mataifa inafanya kazi zake kama kawaida japo kuna matatizo ya hapa na pale.
Amesema kuwa maafisa wa kikosi hicho, raia wa kawaida, wamejikita katika mji mkuu wa Port- au -Prince huku timu zingine ndogondogo za kuhamahama zikichunguza hali ya kisiasa na utawala wa sheria zinazurura mikoa yote 10 huku maafisa wake wakiwasiliana na wananchi pamoja na washika dau wengine.
Pia kikosi cha Umoja wa Mataifa kimetuma maafisa wake sio tu katika vikosi vya polisi lakini pia katika magereza 18 nchini humo.
Amesema kuwa eneo ambalo wametilia mkazo ni kusaidia kukabiliana na watu kuwekwa ndani bila kufikishwa mahamani na vilevile mjazo gerezani.
Hata hivyo ameongeza kuwa tatizo baado ni udhaifu katika taasisi za sheria kuendelea kuzusha changamoto kwani kuna baadhi watu ambao hawaguswi kwa kuchukua hatua za kinidhamu dhidi endapo wametenda makosa.