Biashara yangu imevuka mipaka ya Tanzania- Lydia
Mkutano wa 62 wa kamisheni ya hali ya wanawake CSW ukikunja jamvi hii leo jijini New York, Marekani, mmoja wa washiriki kutoka Tanzania Lidya Jacob amezungumzia mafanikio makubwa aliyopata katika kilimo na biashara hususan k wenye usindikaji wa bidhaa. John Kibego na ripoti kamili.
Akihojiwa na Idhaa ya kiswahili ya Umoja wa Mataifa kando mwa mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake CSW62 jijini New York Marekani, Bi. Jacob amesema mafunzo ya usindikaji aliyopata yeye na wanawake wengine huko Kisarawe yamewasaidia katika kukuza kilimo na biashara ya korosho.
(Sauti ya Lydia Jacob)
Na kuhusu mafanikio aliyoyapata kwa kushiriki kutano wa kamisheni ya hali wa wanawake na pia kupata fursa ya kuonyesha biashara yake ambayo sasa imevuka mipaka ya Tanzania, Bi. Jacob anasema.
(Sauti ya Lydia Jacob)