Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Eh Mola turejeshee furaha yetu- Wakimbizi

Eh Mola turejeshee furaha yetu- Wakimbizi

Pakua

Nchini Sudan Kusini msimu wa mvua ukitarajiwa kuanza, baadhi ya wakimbizi wa ndani na hata wale waliokimbilia nchi za jirani wameamua kurudi nyumbani angalau kuendelea na maisha yao. Assumpta Massoi na taarifa kamili.

(Taarifa ya Assumpta Massoi)

Hapa ni Kajo Keji, mji ulioko jimbo la Equitoria ya Kati nchini Sudan Kusini. Eneo hilo lilikuwa mahame tangu kuanza kwa mzozo nchini humo mwezi disemba mwaka 2013.

Hivi sasa nuru ya amani imewezesha baadhi ya wakimbizi kurejea ili kuendeleza maisha yao na miongoni mwao ni Grace Kobong akikagua lililokuwa shamba lake la mihogo.

(Sauti ya Grace Kobong)

“Napanga kurejea hapa na kuishi. Mwanangu alifariki dunia na sina mtu wa kunisaidia. Alizoea kuja na kunisaidia kuvuna mihogo lakini sasa hayupo. Nimerejea ili nilime na nasaka mbegu za mahindi nipande.”

Tume ya usaidizi na urekebishaji Sudan Kusini iliandaa semina kujadili jinsi ya kusaidia wakimbizi wanaorejea na kusihi jamii ya kimataifa isaidie kwa hali na mali ili hata wakulima waweze kufanya shughuli zao na hivyo kupata chakula.

Grace ana matumaini.

(Sauti ya Grace Kobong)

 “Nina Imani, ninasali ili amani irejee nchini mwetu. Ninaomba ili Mungu atugeuzie uso wake. Hebu na amani irejee kwenye nchi hii.”

Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
1'22"
Photo Credit
UN Photo/Isaac Billy