Usawa wa kijinsia haumaanishi kuwakandamiza wengine
Mkutano wa 62 wa kamisheni ya hali ya wanawake duninai, CSW62, unaoendelea jijini New York, Marekani unaangazia mada mbalimbali na umeweza kuwaongezea maarifa washiriki kutoka nchi mbalimbali.
Mmoja wa washiriki hao ambaye anasema amefaidika na mkutano huo mpaka sasa ni Oliver Kinabo kutoka Da-es Salaam nchini Tanzania.
Akigusia mada ya kumwezesha mwanamke masuala ya kijamii, kiuchumi na siasa ameondoa hofu miongoni mwa wanaume ya kujihisi kuwa jinsia ya kike inataka kuipiku ya kiume kutokana na mkutano wenyewe.
(Sauti ya Oliver Kinabo)
Amekanusha nadharia ya kwamba uwepo wa wanaume kwenye vikao vya wanawake ni sawa na kuwabembeleza wanaume akisema..
(Sauti ya Oliver Kinabo)
Mmoja wa wanawake anaehudhuria mkutano wa CSW62 unaoendela hapa New York , Marekani amesema kuwa wao kudai usawa wa kijinsia sio maana kuwa wanataka kuwakandamiza wanaume.