Neno la Wiki: Halasa
Katika Neno la Wiki hii leo tunaangazia neno “Halasa” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Bwana Sigalla anasema neno "Halasa" katika muktadha wa baharini au uvuvi ni malipo yanayopata mtu baada ya kukatwa gharama na makato mengine yote. Hasala pia ni faida au faida kutokana na mapato ya mtu.
Hasala pia ina maana sawa na yenye nafuu au afadhali, Pia ni yenye kukamilika, timamu, timilifu, au sawasawa.