Wanawake washirikishwe katika utatuzi wa migogoro: Zerrougui
Wakati umefika kuwawezesha wanawake kuhusika katika shughuli za kutatua migogoro mbalimbali.
Hayo yametamkwa na Bi Leila Zerrougui, mkuu wa kikosi cha MONUSCO, kikosi ambacho ni cha Umoja wa Mataifa kinacholinda amani Congo katika mazungumzo yake na UNNews wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Ametoa kauli yake kuhusu mchango wa mwanamake , katika ngazi za uongozi.
(SAUTI YA LEILA)
“Nadhani ni muhimu kuwa na viongozi wanawake katika muktadha kama huu kwa sababu, kwa muda mrefu una wanaume ambao wanajihusisha na migogoro ambayo waathirika wake wakubwa ni wanawake na watoto. Kwa hivyo nadhani mwelekeo wa mwanamke ambae ana uelewa wa kutosha pamoja na ujuzi ni muhimu mno kwa sababu utapata taswira tofauti ya wanaume na wnawake
Amesema kuwa mseto wa mwanamme na mwanamke utaleta msukumo wa jinsi ya kuangalia masuala kwa mitazamo tofauti vile kutilia mkazo waathirika, na kile kinachoweza kupatikana sio tu kupitia mapigano au vita lakini kuwaelewesha wananchi ambao wako katika taifa linalopitia migogoro ya ndani kuwa, ufumbuzi sio tu kupitia mabavu lakini pia kupitia njia za amani.
Mkuu wa kikosi cha MONUSCO ,kikosi cha Umoja wa Matifa kinacholinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Leila Zerrougui ametaka wanawake nao kujumulishwa sawa na wanaume katika majukumu ya kutatua migogoro mbailmabli.