Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wengine wataka kutumia matambara kujisitiri hedhi

Wengine wataka kutumia matambara kujisitiri hedhi

Pakua

Suala la wanawake na wasichana kujisitiri wakati wa hedhi limesalia kuwa kizungumkuti hasa katika nchi maskini zijulikanazo pia kama nchi zinazoendelea. Hii ni kutokana na kwamba katika jamii nyingi za maeneo hayo suala hilo ni mwiko kuzungumzwa  hadharani na pia  pedi za kisasa ambazo hazina madhara ya kiafya ni vigumu kuzimudu kwa kuwa ni ghali. Hii inawalazimu baadhi ya wazazi kuwashauri watoto wao kutumia nguo kuukuu kujisitiri kama njia mbadala. Lakini hilo madaktari wanasema halifai. Kupambanua mvutano huo Siraj Kalyango anakualiaka kwenye Makala hii.

Audio Credit
Siraj Kalyango
Audio Duration
3'59"
Photo Credit
Nchini Ethiopia kiwanda kidogo cha kutengeneza taulo za kike na kimesaidia kupunguza madhila kwa wanawake na watoto wa kike. (Picha:©UNICEF/2016/Carazo)