Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wachuuzi wa samaki Burundi na mafunzo ya kuepusha uchafuzi wa mazingira

Wachuuzi wa samaki Burundi na mafunzo ya kuepusha uchafuzi wa mazingira

Pakua

Ziwa  Tanganyika kwenye ukanda wa Maziwa Makuu barani Afrika, limekuwa mashuhuri sio kwa kusafirisha watu na bidhaa bali pia katika kuzalisha  samaki  aina mbalimbali  Lakini changamoto kubwa ni uhifadhi za samaki  baada ya kuvuliwa hadi kuliwa ili kuepusha uchafuzi wa mazingira. Ingawa samaki huonekana  kwa wengi kama chakula bora, lakini kama hawatahifadhiwa vyema wanaweza kusababisha madhara makubwa  kwa watumiaji na mazingira. Hivi karibuni , wavuvi na wauzaji wa samaki mjini Bujumbura nchini Burundi walihamasishwa jinsi ya kuhifadhi vyema samaki  kwa matumizi ya mlo lakini pia kuhakikisha wanahifadhi mazingira kwa kutotupa hovyo samaki walioharibika.. Katika makala hii mwandishi wetu wa maziwa Makuu Ramadhani Kibuga amezungumza na wachuuzi wa samaki sokoni CoTeBu ili kufahamu  mbinu wanazotumia   kuhifadhi samaki wao.

Audio Credit
Selina Jerobon na Ramadhani Kibuga
Audio Duration
4'17"
Photo Credit
Uvuvi bora sambamba na viwanda vya kuchakata samaki ni mojawapo ya mbinu za kuinua uchumi wa kaya na taifa kwa ujumla.