Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Radio haifi ng'o

Radio haifi ng'o

Pakua

Ujumbe wa siku ya radio duniani mwaka huu wa 2018 ni Radio na Michezo! Umoja wa Mataifa unataka chombo hicho adhimu kitumike kusaidia watu kuchanua na kuonyesha uwezo wao wote. Miongoni mwa watu ambao radio imeweza kuibua stadi zao ni Jane John, mtangazaji wa kike wa habari za michezo katika shirika la utangazaji nchini Tanzania, TBC. Assumpta Massoi alizungumza na Jane kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam, Tanzania na kuanza kwa kumuuliza manufaa ya radio!

Audio Credit
Siraj Kalyango na Assumpta Massoi
Sauti
5'10"
Photo Credit
Jane John (TBC-Tanzania)