Neno la wiki - Ndongosa
Pakua
Wiki hii tunaangazia neno "Ndongosa" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Bwana Sigalla anasema neno “Ndongosa” ni ng'ombe wa kike ambaye anatoka kwenye hali ya undama kuingia ukubwa lakini bado hajapandwa.