Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kazi ni kazi bora mkono uende kinywani

Kazi ni kazi bora mkono uende kinywani

Pakua

Vijana hutumia mbinu mbalimbali ili kukidhi  mahitaji ya maisha yao ya kila siku na fani ya ulimbwende au uanamitindo imekuwa ni moja  ya  fani zinazowavutia vijana , kwanza ikiwajengea umaarufu mkubwa lakini pia kuwasaidia kuwa na ajira ya kikidhi mahitaji yao. Hakimu Nkengurutse kijana wa miaka 21 kutoka vijijini  nchini  Burundi amevuka mito na bahari na kutua  nchini Afrika ya Kusini ambako anakofanya kazi ya uanamitindo.

Na baada ya kufanikiwa kwenye kazi hiyo, Hakim sasa anatumia muda wa mapumziko  katika nchi yake ya asili  Burundi ili kuwachagiza vijana wenzie kuchangamkia  faini hiyo ambayo imegeuza Maisha yake. Kufahamu zaidi safari ya mafanikio yake ungana na mwandishi wetu wa Maziwa Makuu Ramadhani KIBUGA katika Makala hii.

Photo Credit
Kijana Hakimu Nkengurutse raia wa Burundi anayefanya kazi ya uanamitindo au ulimbwende nchini Afrika Kusini. Picha kwa hisani ya :Hakimu Nkengurutse