Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kutoka Nigeria hadi Hungary, kulikoni?

Kutoka Nigeria hadi Hungary, kulikoni?

Pakua

Ama kweli wahenga walinena kuwa mchumia juani, hulia kivulini na methali hiyo imedhihirika kwa raia mmoja wa Nigeria ambaye baada ya kupitia machungu mengi kwenye mikono ya wasafirishaji haramu, sasa ametulia tuli. Ndoto yake ya kufika Ulaya ilitimia na sasa ana ndoto kubwa zaidi. Kutimia kwa ndoto yake kunaenda sambamba na kile kinachopigiwa chepuo kila siku na Umoja wa Mataifa kuwa uhamiaji au wahamiaji si mzigo bali ni lulu inayopaswa kulindwa kwani huleta nuru kwenye giza. Je nini kimetokea kwa mhamiaji huyu huko Nigeria? Siraj Kalyango anafafanua kwenye Makala hii.

Photo Credit
Rita Joy Osazee mkimbizi kutoka Nigeria akihudumia wazee nchini Hungary. Picha: UM/Video capture