WHO yatoa tani 70 ya vifaa vya Hispitali Yemen
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO, limepeleka tani 70 za misaada ya kibinadamu ikiwemo vifa upasuaji kwajili ya hospitali katika mji mkuu Sana huko Yemen.
Msaada huu ambao ni mkubwa zaidi kupelekwa chini Yemen tangu mwaka huu uanze, utasaidia mahitaji ya wagonjwa wapatao 2000 ambao ni wagonjwa wa akili na upasuaji, na pia magonjwa yanaohitaji uangalizi wa maadabara.
Dr Nevio Zagara ambaye ni mwakilishi wa WHO Yemen amesema , jitihada za WHO kupeleka vifaa za matibabu Yemen, ni hatua nzuri katika kuziwezesha hospital za Yemen ambazo zimelemewa na wagonjwa wengi lakini huduma hazitoshelezi kutokana na uwezo mdogo wa kuwahudumia wagonjwa.
Aidha Dr Nevio amesema japo hali ya usalama ni hatarishi kwa watoa huduma wa WHO na mashirika mengine ya kimataifa, bado WHO ina wajibu wakusaidia huduma za afya nchi nzima ili kuokoa maisha ya mamiolini ya wananchi wasio na hatia .