Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tumesikitishwa na kushtushwa na shambulio dhidhi ya walinda amani wetu:Mahiga

Tumesikitishwa na kushtushwa na shambulio dhidhi ya walinda amani wetu:Mahiga

Pakua

Tumeshtushwa sana na kusikitishwa na shambulio la jana dhidi ya walinda amani wetu. Amesema hayo waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika ya Mashariki wa Tanzania Balozi Augustine Mahiga alipozungumza leo na Flora Nducha wa idhaa hii kufuatia kuuawa kwa walinda amani wa Tanzania 14, wengine 38 kujeruhiwa wakiwemo walio hali mahtuti na wanne kutojulikana walipo huko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, baada ya kundi la waasi wa ADF kuzamia kituo cha walinda amani hao.

(MAHOJIANO KATI YA FLORA NDUCHA NA BALOZI AUGUSTINE MAHIGA)

Photo Credit
(Picha:UN/Aliza Eliazarov)