Usawa wa kijinsia katika ajira kuongeza pato la dunia kwa 26%: Phumzile
Shirika la Umoja wa Mataifa la wanawake UN Women, kwa kushirikiana na shirika la maendeleo la wananwake NAMA huko Sharjah Falme za kiarabu, wamezindua kongamano la kimataifa la siku mbili kuanzia leo tarehe 4 hadi 5 desemba.
Lengo la kongamano hilo ni kuhamasisha serikali na asasi za kiraia kuwashirikisha wanawake katika maendeleo ya kijamii ikiwa ni sehemu ya kampeni ya siku 16 ya kupinga ukatili dhidi ya wananake duniani.
Mgeni rasmi Mrugenzi wa UN Women Phumzile Mlambo-Ngcuka amepongeza juhudi za NAMA kuandaa kongamano linalowapa wanawake jukwa la kimataifa katika kujenga fursa za biashara kwa wanawake, kushirikiana na makampuni, serikali na wajasiriamali, na pia kujenga ushirikiano kati ya Falme za kiabu, Afrika Kusini na nchi nyingine.
Bi Phumzile amesema uwezeshaji kiuchumi kwa wanawake ni muhimu katika maisha endelevu na kiuchumi, akitolea mfano wa uchunguzi wa hivi karibuni ulioonyesha kama wanawake watapewa jukumu sawa katika masoko ya ajira na wanaume , pato la uchumi wa dunia litaongezeka kwa asilimia 26 ambapo ni sawa na kiasi cha dola trillion 28 ifikapo mwaka 2025.