UM walaani shambulizi la kigaidi Baghdad
Pakua
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq, Ján Kubiš amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea usiku wa kuamkia leo kwenye mji mkuu Baghdad na kusababisha vifo vya raia 12 na kujeruhi wengine wengi.
Bwana Kubis metuma salamu za rambirambi kwa wafiwa na pia serikali ya Iraq huku akiwatakia ahueni majeruhi.
Pia ameitaka serikali ya Iraq ifanye uchunguzi kubaini wahusika ili wachukuliwe hatua za kisheria haraka iwezekanavyo.
Aidha Bwana Kubis ameonya serikali ya Iraq kuwa ingawa ISIL wameshindwa na majeshi ya Iraq bado wataendelea kuwa tishio kwa maisha ya wananchi wa Iraq kila uchao.